October 14, 2014


Yanga imeendelea kujifua jijini Dar es Salaam na nahodha wake amesema wako fiti na hakuna majeruhi hata mmoja.


Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amesema wachezaji wako ngangari na wanaendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Boko Veterani jijini Dar es Saalaam.
“Tuko vizuri tunashukuru na mazoezi yanaendelea vizuri pia.
“Lengo ni kufanya vizuri, hivyo tunajituma,” alisema Cannavaro ambaye anajiunga na Yanga baada ya kuitumikia Taifa Stars kiufasaha na kuifungia bao wakati ikiitungua Benin kwa mabao 4-0 katika mechi ya kirafiki, juzi.

Yanga inajiandaa na mechi dhidi ya watani wake Simba, Oktoba 18.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic