Khalid Nzokwa, Bukoba
Kadi nyekundu aliyolambwa nahodha wa Yanga,
Nadir Haroub ‘Cannavaro’ imesababisha
tafrani kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini hapa.
Cannavaro alipewa kadi nyekundu baada ya
kumfanyia madhambi Paul Ngwai ambaye alifunga bao la pekee katika mechi hiyo
wakati Yanga ikilala kwa bao 1-0.
Mashabiki hao walicharuka na kutaka kumvamia
mwamuzi, hali iliyosababisha askari polisi kuingia kusaidia.
Mashabiki hao walilalama kwamba mwamuzi
hakuwa na sababu ya kutoa kadi hiyo.







0 COMMENTS:
Post a Comment