November 8, 2014


Kocha Mkuu wa Simba, Mzambia, Patrick Phiri, ametamka kwa kujiamini kuwa, kiungo wake mkabaji, Jonas Mkude, amesaini Simba mkataba wa miaka miwili na Yanga wasahau nyota huyo kusaini huko.


Kauli hiyo inaonekana kupishana na ya kiungo mwenyewe ambaye anadai yeye hadi hivi sasa hajasaini Simba huku akitoa nafasi kwa klabu zinazomhitaji kumfuata kwa ajili ya kufanya mazungumzo ili asaini kwenye msimu ujao.

Kwa mujibu wa kanuni za Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), kiungo huyo anaruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu inayomhitaji kutokana na kubakiza miezi sita kwenye mkataba wake.

Phiri alisema kuwa ana uhakika mkubwa wa Mkude kusaini Simba, hivyo amewaondoa hofu mashabiki kuhusiana na mchezaji huyo kwenda Yanga.

Phiri alisema, ni ngumu kwa kiungo huyo kuondoka Simba hata kama bado hajasaini kutokana na umuhimu mkubwa alionao kwenye kikosi chake hicho.
Mzambia huyo aliongeza, tayari amewaonya viongozi wa timu hiyo kwa kuhakikisha wanawabakiza wote anaowahitaji ambao mikataba yao inaelekea ukingoni kumalizika.

“Nikupe siri moja, Mkude amesaini Simba na hizo taarifa za kwenda huko Yanga ni uongo, mimi ninakuthibitishia hilo, kama unabisha tusubiri tuone kwenye usajili ujao.


“Ni ngumu kumuachia mchezaji mwenye umuhimu ambaye anapata nafasi kwenye kikosi cha kwanza kwenda kuichezea timu nyingine tena kwa wapinzani wetu wakubwa Yanga.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic