November 8, 2014


Mchezaji bora wa mwezi Oktoba ambaye ni kiungo wa Klabu ya Azam, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, leo anatarajiwa kukabidhiwa tuzo yake wakati timu yake itakapokuwa kwenye uwanja wake wa nyumbani Azam Complex, Chamazi kumenyana na Coastal Union.


Sure Boy alichaguliwa kuwa mchezaji bora baada ya kupata kura nyingi kutoka kwa wataalamu waliowekwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) katika kila mechi ili kumchagua mchezaji bora wa mechi kisha mwisho wa mwezi kuchaguliwa mchezaji bora.
Mkurugenzi wa  mashindano wa shirikisho hilo, Boniface Wambura, alisema kuwa mchezaji huyo atakabidhiwa tuzo hiyo kabla ya mchezo wao utakaowakutanisha na Coastal Union.
“Mchezaji huyo atakabidhiwa zawadi yake kutoka kwa mdhamini wa ligi ambayo ni tuzo pamoja na fedha shilingi milioni moja, atakabidhiwa kabla ya mechi,” alisema Wambura.

Wakati huohuo, shirikisho hilo limetangaza rasmi tarehe ya kufunguliwa kwa dirisha dogo la usajili ambalo linatarajiwa kufunguliwa ifikapo Novemba 15 hadi Desemba 15, mwaka huu.


“Pia tunazitangazia klabu kuwa dirisha dogo la usajili litafunguliwa rasmi mwezi huu tarehe 15 na litaenda mpaka kufikia mwezi ujao, Desemba 15 ni muda wa kila timu kufanya usajili ili kuimarisha vikosi vyao kwa ajili ya mzunguko wa pili,” alisema Wambura.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic