December 8, 2014


Kiungo mpya mkabaji mpya wa Yanga, Mbrazili, Emerson De Oliviera, amewaangalia viungo wenzake, Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Said Juma na kutamka kuwa ana kibarua kigumu cha kupata namba kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Marcio Maximo.


Emerson alitoa kauli hiyo wikiendi iliyopita mara baada ya mechi ya kirafiki kati ya Yanga na Express ya Uganda kumalizika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar. Yanga ilishinda bao 1-0.

Emerson amesema atapata kibarua kigumu kutokana na uwezo mkubwa wa viungo hao aliowakuta kwenye kikosi hicho baada ya kuwaona mazoezini na kwenye mechi dhidi ya Express.

Alisema amepanga kuongeza bidii ya mazoezi kuhakikisha anamshawishi kocha wake aingie kwenye kikosi cha kwanza, baada ya kuishuhudia mechi dhidi ya Express akiwa jukwaani.

 “Yanga nimekuta ushindani mkubwa wa viungo, ni timu yenye wachezaji wenye kasi na viwango vikubwa ambao ninaamini watanipa ushindani wa namba.

“Lakini hiyo hainipi hofu ya mimi kuingia kwenye kikosi cha kwanza, ninaamini nina uwezo mkubwa wa kucheza nafasi ya kiungo, kikubwa nilichopungukiwa ni pumzi na stamina, vitu ambavyo nilivifanyia kazi katika mazoezi ya wiki iliyopita.

“Mchezaji kama Niyonzima, Twite na Said niliowaona mazoezini na kwenye mechi, wote wana viwango vya kustahili kuanza kwenye kikosi cha kwanza, hivyo nina kazi kubwa ya kumshawishi kocha anipange,” alisema Emerson.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic