December 8, 2014



Uongozi wa Simba umeamua kuachana na harakati za kutaka kumsajili kiungo mshambuliaji, Mgambia, Omar Mboob ambaye alikuwa anafanya majaribio ya wiki mbili na kikosi hicho kwa kile kinachosemekana kuwa uongozi wa timu hiyo kwa sasa hautaki kumuacha mchezaji yeyote.


Mboob ambaye alitua nchini wiki iliyopita akitokea Semgar FC ya nchini Gambia, alifanikiwa kuitumikia timu hiyo katika michezo kadhaa ukiwemo ule dhidi ya kikosi cha vijana.

“Viongozi wameamua kuachana na suala la kumsajili Mboob ambaye alikuwa anafanya majaribio na kikosi hicho kwa kuangalia kigezo cha kutotaka kuwaacha wachezaji wengine wa kigeni kutokana na umuhimu wao kwa sasa ndani ya kikosi.

“Ila ameambiwa anaweza tena kurudi Simba kama akitaka kusajiliwa katika kipindi cha usajili wa mwanzo wa msimu ambapo hapo viongozi watakuwa wanajua nani wamuache ili yeye apate nafasi ya kusajiliwa,” kilisema chanzo chetu.

Alipotafutwa Mwenyekiti wa kamati ya usajili wa timu hiyo, Zacharia Hans Poppe ambaye hakuwa tayari kukubali au kukataa kuhusiana na ishu hiyo.
“Siwezi kusema lolote kuhusiana na jambo la kuachwa kwa Mboob kwa kuwa bado sijapewa taarifa yoyote na viongozi wengine kuhusiana na mchezaji huyo,” alisema Hans Poppe.
Lakini kabla, Hans Poppe alisema: "Mboob si kwamba tulikuwa tunamhitaji, kuna wakala wake yuko huko Spain ndiyo aliomba aje tumuangalie.

"Kama tukiona kiwango chake kiko juu sana tofauti na wachezaji tulionao, basi tunaweza kumsajili. Vinginevyo tunaweza kumuacha aende, halafu tutaangalia wakati wa usajili wa mwanzo wa msimu."


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic