December 8, 2014


Kitasa mpya wa Mbeya City, Juma Nyosso, amefunguka kuwa amefurahi kujiunga na timu hiyo lakini kubwa alilonalo kwa sasa ni kupambana kurejesha heshima ya timu hiyo iliyopotea hivi karibuni.

Beki huyo wa zamani wa Simba na Coastal Union, amejiunga na timu hiyo hivi karibuni kwa mkataba wa mwaka mmoja akiwa mchezaji huru baada ya kukaa nje ya michuano ya Ligi Kuu Bara kwa takribani miezi mitano.

Nyosso alisema kuwa kikubwa kwake kwa sasa pamoja na wachezaji wenzake ni kuhakikisha wanairejesha timu hiyo katika hadhi yake ya awali kwa ajili ya kupata mafanikio stahiki ya kitimu, kisha ya kwake binafsi yatafuata.

Mbeya iliyokuwa moto wa kuotea mbali msimu uliopita na kumaliza nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi, safari hii imekuwa na matokeo ya kusuasua na kuishia kuburuza mkia baada ya mechi saba za awali za ligi.

“Nimefurahi kurejea kwenye ligi lakini kikubwa kwa sasa ni kuhakikisha naisaidia vilivyo timu yangu ili irejeshe heshima yake, naamini tutashirikiana vema na wachezaji wenzangu katika hili, timu ikishakaa pazuri, heshima ya mchezaji mmojammoja itakuja baadaye,” alisema Nyosso, beki wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars.  


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic