STAND UNITED. |
Pambano
la Ligi Kuu Bara kati ya Mtibwa Sugar dhidi ya Stand United, limeahirishwa.
Pambano
hilo limeaahirishwa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha mjini Turiani na
kusababisha Uwanja wa Manungu kujaa maji.
Awali
pambano hilo lilisimama kwa dakika 15, lakini kamisaa Bile Mwilima alipoona
alama za uwanja zimefutika, pamoja na utelezi kuwa wa hali ya juu, akatangaza
kuliahirisha.
Kutokana
na hali hiyo, pambano hilo ambalo hadi linavunjika lilikuwa sare ya bila mabao,
litachezwa kesho saa mbili asubuhi.
Kwa
mujibu wa kamisaa huyo pambano hilo litachezwa kesho kuanzia dakika ya 6.
0 COMMENTS:
Post a Comment