Uongoziwa Klabu ya Yanga umefunguka kuwa upo tayari kuweka kambi Chamazi kufuatia ofa
waliyoitoa Azam ya kuwataka wakaweke kambi huko kwa ajili ya kujiandaa na
mchezo wa raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri.
Inaelezwa
kuwa wiki iliyopita uongozi wa Azam FC ulikataa ombi la Al Ahly kuweka kambi
kwenye eneo lao hilo pindi watakapokuja nchini kucheza dhidi ya Yanga katika
hatua hiyo baada ya kufanikiwa kuitoa Komorozine.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Bin Kleb amesema hawawezi kuiachia ofa kama hiyo kwa kuwa mtazamo wao ni kuona wanafanikiwa
kufanya vizuri katika mechi hiyo.
“Mtu
yeyote hawezi kukataa ofa kama hiyo, iwapo Azam wameamua kutusaidia sisi tupo
tayari ila tunamsikiliza mwalimu Hans Van Pluijm anahitaji kambi ya aina gani
ili kuweza kujiandaa.
“Mwalimu
ndiye anayejua aina ya timu anayotarajia kukutana nayo, hivyo uongozi
unamwachia kila kitu na yeye ndiye atakayetoa maamuzi,” alisema Bin Kleb.
0 COMMENTS:
Post a Comment