December 7, 2014


Kocha mkongwe nchini, Abdallah Kibadeni ameonya wale wanaotoa taarifa bila ya kuwa na uhakika.

Kibadeni amesema amesitikishwa sana na usumbufu walioupata watu jana kwa yeye kuzushiwa kifo.

“Kweli imenisikitisha sana, ndiyo maana nimeamua kusema tena. Si jambo jema na vizuri mtu ukiambiwa kitu uulize kupata uhakika.

“Kutangaza kifo cha mtu si jambo dogo, pia si sahihi kama hauna uhakika.

“Hivyo nawaasa watu kuhakikisha jambo kabla ya kulitangaza au kuandika. Nimeambiwa kuna mtandao ndiyo ulianzisha hilo jambo, basi vizuri watu wafuate weledi,” alisisitiza Kibadeni.

Jana zilizagaa taarifa kwamba Kibadeni amefariki dunia jambo ambalo si kweli.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic