December 7, 2014


Kiatu kilichofunga bao katika fainali ya Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil kimeuzwa kwa uero milioni 2 (Sh bilioni 4.2).


Kiatu hicho ni mali ya mshambuliaji wa Ujerumani, Mario Gotze ambaye alifunga bao hilo pekee na kuiangusha Argentina kwa bao 1-0.

Kiatu hicho kiliingizwa kwenye mnada maalum, kiuzwe na fedha zake zitumike kusaidia watoto wenye matatizo.
Gotze ambaye hakuwahi kukisafisha kiatu hicho tokea fainali, alikubali fedha ziwasaidie watoto kupitia mradi wa 'A Heart for Children', lakini hakuna aliyejua kitafikia bei hiyo.
Hali hiyo imeonyesha kuwashangaza wengi lakini imezidi kuonyesha kiasi gani mpira una nguvu.





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic