December 6, 2014


KESSY.
Beki wa kulia wa Mtibwa Sugar, Hamis Kessy, amefunguka kuwa baada ya kuwatajia dau la shilingi milioni 35, Simba, ambayo inamuwania kumsajili, viongozi wa kikosi hicho wala hawajarudi tena kuzungumza naye.


Simba ina uhaba wa beki ambapo haikufanya vizuri katika mechi saba za mwanzo na kujikuta ikitoka sare mechi sita na ikishinda moja tu.

Kessy amesema kuwa, kuna viongozi wa Klabu ya Simba ambao walimfuata wakitaka kumsajili kwa ajili ya kuichezea timu hiyo msimu ujao lakini amewapa sharti la kuhakikisha wanampa milioni 35 na kama itashindikana basi hatakubali kuondoka katika klabu yake hiyo ya sasa.

“Mimi nilifuatwa na Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange ‘Kaburu’ kutaka kunisajili na nikawataarifu kuwa dau langu ninalolihitaji ni shilingi milioni 35, hivyo hawajarudi kuzungumza na mimi tena.


“Kuhusu upande wa viongozi wenyewe wameniruhusu kwani walikuwa wakisubiri majibu yangu na kuona kama nimeridhika kuondoka na wala hawana tatizo na wanachotaka wao ni taratibu kufuatwa,” alisema Kessy.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic