Kwenye michezo suala la thamani ya kitu au
jambo, inapewa kipaumbele sana. Kwamba nani analipwa mshahara zaidi, timu ipi
ina fedha zaidi au mdhamini yupi anamwaga fedha nyingi zaidi.
Kwa upande wa wadhamini wanaomwaga fedha
nyingi kwenye timu kubwa za Ulaya ni pamoja na Fly Emirates wa Real Madrid na
Arsenal. Usiwasahau Qatar Foundation wa Barcelona, Chevloret wa Man United , Samsung
wa Chelsea, Deutche Telekom wa Bayern Munich na wengine.
Makampuni hayo yanakubali kutoa mamilioni ya
fedha kwa kuwa yanajua yatafaidika na matangazo wakati timu hizo zikicheza.
Wachezaji wa timu husika huvaa matangazo hayo vifuani mwao.
Wachezaji wanaweza kuvaa matangazo karibu
kila sehemu ya jezi au bukta zao. Lakini kifua ndiyo ghali zaidi kwa kuwa
anawekwa mdhamini mkuu.
Hilo ndilo lililonivutia kuandika Metodo ya
leo baada ya kumuona Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Jakaya Mrisho
Kikwete akiwa amevaa jezi ya zamani ya Real Madrid akifanya mazoezi.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari jana,
Kikwete ameshauriwa na madaktari kufanya hivyo baada ya ule upasuaji
aliofanyiwa nchini Marekani. Hivyo akiwa na wasaidizi wake, picha zilionekana
akiwa amevaa jezi hiyo ya zamani ya Real Madrid ikiwa na tangazo la Beanq-Siemens
yenye asili yake nchini Ujerumani.
Kama unakumbuka ile Madrid ya enzi ya akina
Ronaldo di Lima, David Beckham, Figo na Zinedine Zidane waliokuwa wakivaa jezi
hiyo na Siemens ambayo ni kampuni ya masuala ya umeme na mitambo mkubwa ikawa
inalazimika kumwaga hadi dola milioni 118 (zaidi ya Sh bilioni 200) ili itangazwe na Real Madrid
kwa misimu mitatu.
Mara baada ya kuiona picha hiyo, nikajiuliza
vipi rais wetu avae jezi hiyo na kuitangaza kampuni hiyo ambayo ilipotaka
kutangazwa na Beckham au Zidane ililazimika kutoa mamilioni ya fedha?
Nikajijibu, Rais Kikwete ni shabiki wa Real
Madrid. Lakini swali jingine likaibuka, hivi ni sahihi yeye kuvaa jezi yenye
tangazo na kutokea hadharani? Kwani nini isiwe na ujumbe mwingine kama “ukimwi
ni hatari”, “pambana na malaria” au “pambana na unyanyasaji wa wanawake na
watoto”?
Naweza nikapishana na wengine, lakini
ninaamini kifua cha Rais Kikwete ni ghali zaidi kwa Watanzania kuliko hata cha
akina Beckham. Hivyo kama ni shabiki wa Madrid, basi angeweza kuivaa jezi hiyo
kwa wakati wake na si pale anapotokea hadharani.
Akiivaa Saleh Ally ambaye naye ni shabiki wa
Madrid, wala haina shida, nani anamjua? Tena ilifikia wakati nikasema bora Rais
Kikwete angevaa jezi ya Taifa Stars, au hata Yanga, si wote tunajua ni
Mwanajangwani. Najua ya Myama hawezi kutinga.
Kwa kifupi, iko haja ya kudhamini kifua cha
kiongozi wetu mkubwa na kuangalia kwa umakini sana anavaa nini.
Ikitokea siku kampuni fulani ya mitambo,
utengenezaji simu au masuala ya umeme, ikagombea tenda na Siemens halafu
ikashindwa, inaweza kuona tofauti.
Huenda inaweza isiuchukulie ushindani ule
kama wa kitaalamu na kawaida. Badala yake ikaanza kuwaza kuna upendeleo kwa
kuwa Rais Kikwete aliwahi kuonyesha wazi anaiunga mkono kampuni hiyo.
Katika ushindani, kawaida wengi hasa wale
wenye tabia ya kutaka kushinda kwa dhati, huwa hawakubali kilahisi na hasa kama
wanajiamini kutokana na ubora wao.
Hivyo ni lahisi sana kwa serikali yetu
kuingia kwenye mitego au hisia za kujaribu kufikiri ni hivyo kwa kuhakikisha
rais wetu havai nguo za matangazo ya makampuni fulani.
Najua yeye kwa England ni shabiki wa
Newcastle, fumba macho ujaribu kufikiria hili. Mfano angekuwa shabiki wa
Liverpool, halafu akavaa jezi yenye mdhamini wao wa sasa, siku chache baadaye
ishu ya Escrow imeibuka na benki hiyo inahusishwa kutokuwa makini. Unafikiri
mngesemaje? Mgefikiraje?









Kumbe kuna wakati Saleh akili yako inafanya kazi vizuri,hongera kwa kuwafumbua macho watanzania maana waandishi wengine wamakalia kuitangaza picha tuu bila kujali matokeo yake
ReplyDeleteVery informative post! There is a lot of information here that can help any business get started with a successful social networking campaign. metodo fanart 2.0
ReplyDelete