Klabu ya Mbeya City
imezindua rasmi njia mpya ya uuzaji wa jezi pamoja na sweta za klabu hiyo, kwa
kuagiza kwa njia ya mtandao kisha kulipia benki yoyote hapa nchini inayotumia
Visa kadi.
Klabu hiyo msimu uliopita
ilifanikiwa kuuza jezi kutokana na timu hiyo, kujizolea mashabiki wengi baada
ya kuanza vyema ligi na kumaliza katika nafasi ya tatu lakini msimu huu
inashika mkia kwenye ligi.
Katibu wa timu hiyo,
Emmnuel Kimbe, amesema wameamua kufanya hivyo ili kupunguza ule upenyo wa jezi feki kuzagaa mitaani.
“ Tumezindua mpango wetu mpya wa uuzaji wa jezi na safari hii
tumeleta na sweta ambazo shabiki popote pale alipo ndani au nje ya nchi ataweza
kununua kwa njia ya mtandao akiwa na visa kadi ambayo ataitumia katika benki
yoyote, jezi bei yake ni 20,000 na sweta 30,000.
“Na hii tumefanya hivi
kutokana na kupunguza lile wimbi la kuuza jezi ambazo sio halali,”alisema Kimbe.
0 COMMENTS:
Post a Comment