Straika wa zamani wa Simba,
Mrundi Amissi Tambwe, amemtetea mshambuliaji mpya wa timu hiyo, Mganda Danny
Sserunkuma, kuwa atawika sana kwenye klabu hiyo.
Tambwe ambaye amejiunga na
Yanga hivi karibuni akitokea Simba amefikia hatua hiyo baada ya mashabiki wa
timu huyo kuanza kumtupia lawama kuwa hana lolote kutokana na kiwango cha chini
alichokionyesha kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar.
Katika mechi hiyo
iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Simba ilitandikwa bao
1-0 huku Sserunkuma akionyesha kiwango kibovu.
Tambwe amesema Simba wasikate tamaa kwani kufanya hivyo ni mapema mno.
”Sserunkuma siyo mchezaji
mbaya ni mchezaji mzuri sana ila tu Simba wanatakiwa kumpa muda na wasianze
kumkatisha tamaa mapema akashindwa kucheza.
“Naamini kabisa wakiwa
wavumilivu atawasaidia kwa sababu ni mmoja kati ya washambuliaji wazuri katika
ukanda huu wa Afrika Mashariki Kati,” alisema Tambwe.
0 COMMENTS:
Post a Comment