December 6, 2014


Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, amesema wanafanya usajili kwa umakini kurekebisha kikosi, lakini akasisitiza waamuzi lazima wachezeshe kwa haki.


Hans Poppe akaenda mbali zaidi kwa kusema katika mechi saba za Ligi Kuu Bara, waamuzi walichemsha huku akitolea mfano wa bao moja la kiungo wa Yanga, Simon Msuva kwamba alipewa tu na mwamuzi.

Hans Poppe alisema katika mechi ya Yanga ilipokuwa ikiivaa Mgambo JKT na Msuva kufunga mawili, moja halikuwa halali.

“Tunaweza kusajili timu nzuri, lakini kama waamuzi hawatakuwa ‘fair’, basi ni kazi bure. Nawaasa wawe fair ili kila timu ishinde kwa uwezo wake na ndiyo maana ya kusajili timu bora.

“Katika mechi kadhaa niliona Simba tukibaniwa makusudi, mfano mechi yetu na Yanga. Kwa makusudi mwamuzi alimuachia yule Jaja, akabaki na kipa lakini akapaisha.

“Lakini niliona mechi ya Yanga dhidi ya Mgambo, nilikuwa naangalia kwenye runinga. Ajabu kabisa bao alilofunga yule kijana Msuva halikuwa halali.

“Kabla hajafunga, kipa wa Mgambo alivamiwa na watu wawili, kila mmoja aliona, mwamuzi akamuacha Msuva afunge.

“Bao jingine la Msuva siku hiyo, sina shida nalo. Watu walisema aliotea lakini mimi niliona lilikuwa ni clean goal (bao safi),” alisema Hans Poppe na kuongeza.

“Mechi yetu na Coastal, hadi wanakwenda kupata faulo ya bao la pili, mwamuzi aliashiria vitendo tofauti, watu wakasimama.

“Lengo si kumsema mtu au vipi, hii ni mifano michache. Ninashauri waamuzi wabadilike, waachane na mambo ya kukiuka sheria na hii inapunguza morali na ushindani wa ligi.”


Hans Poppe alisisitiza Simba inaendelea kumalizia usajili katika sehemu kadhaa kwa ajili ya kujiimarisha zaidi ili kumaliza msimu ikiwa sawasawa.

1 COMMENTS:

  1. Tayari Hanspope kashachanganyikiwa maana taarifa ya kufungwa goli 4 siku ya mtani jembe anazo!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic