December 5, 2014

MHARIRI KIONGOZI WA GAZETI LA CHAMPIONI, SALEH ALLY (KUSHOTO) AKIHESABU SIMU TANO ZA MASAU BWIRE. KULIA NI MHARIRI WA CHAMPIONI JUMAMOSI, SHABANI MBEGU NA MWENYE SUTI NI MHARIRI WA CHAMPIONI JUMATANO, PHILLIP NKINI.

Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire, inawezekana ndiye anayeongoza kwa kuwa na simu nyingi kati ya wasemaji wote hapa Tanzania.


Msemaji huyo mwenye mbwembwe nyingi, anamiliki simu tano za mitandao yote ambayo inapatikana hapa nchini na anasema hata ukiingia mtandao mwingine atanunua simu nyingine.

Masau amesema  anamiliki simu hizo kwa kuwa hataki sana usumbufu na analahisisha watu kumpata.
 
HII NI MWAKA JANA, ALIKUWA ANAMILIKI SIMU TATU.
“Ninamiliki simu tano kama unavyoona. Unajua kila mtandao nina simu yake, Tigo, Zantel, Airtel, Vodacom na Smart, ndiyo maana unaona ninamiliki simu nyingi.

“Hapa nawapa hata waandishi urahisi wanaponitafuta kwa ajili ya stori,” alisema.

Alipoulizwa kwa nini asitumie simu zenye laini mbili na kuendelea alijibu: “Hapana, napenda sana simu zenye laini moja, naamini hizi ndiyo imara hata kama utaongezeka mtandao mwingine kesho nitanunua simu nyingine.”

Awali, Masau alikuwa anamiliki simu mbili, zikaongezeka ahdi tatu na sasa zimefikia tano!


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic