Kocha Mkuu wa Simba,
Mzambia, Patrick Phiri ametangaza kuwa kwa sasa ni kipindi cha kumtumia zaidi
Mganda, Juuko Murushid, ambaye atakuwa akisaidiana na Hassan Isihaka katika
safu ya beki wa kati.
Kauli hii ya Phiri
inamaanisha kuwa sasa nahodha, Mganda, Joseph Owino hana lake tena kwenye kikosi
hicho.
Owino amejikuta akianzia
benchi katika mechi mbili muhimu, dhidi ya Yanga katika mchezo wa Nani Mtani
Jembe 2, kabla juzi Ijumaa kuachwa kwenye kikosi cha kwanza katika mchezo dhidi
ya Kagera Sugar ambapo Simba ilikufa bao 1-0.
Phiri amesema, :“Sina tatizo lolote na Owino na wala siyo kwamba
anaumwa, ukiangalia safu yetu ya ulinzi wa kati ina watu watatu, lakini Juuko
(Murushid),anahitaji kupata mechi nyingi ili apate uzoefu wa ligi, pia bado
naangalia kama kombinesheni yake na Isihaka inaweza kukaa vizuri hivyo ni
vizuri akicheza sana.”
Nyota ya Owino iling’ara
msimu uliopita akiwa pacha ya Mkenya, Donald Musoti, ambaye hata hivyo
alienguliwa, pengo lililotajwa kuitafuna Simba mpaka sasa.
0 COMMENTS:
Post a Comment