December 5, 2014

KESSY (KUSHOTO) AKIPAMBANA NA TSHABALALA WA SIMBA.
Uongozi wa Klabu ya Simba umefunguka kuwa, upo katika hatua za mwisho za kumalizana na beki namba mbili wa Mtibwa Sugar, Hamis Kessy licha ya kuripotiwa kuwepo kwa ugumu wa mchakato huo wa usajili.

Hata hivyo kumekuwa na taarifa kwamba mazungumzo yako katika hatua nzuri sana na pande zote mbili, yaani Simba na Mtibwa Sugar zimekubali kwamba zimefanya mazungumzo.


Simba ambayo imeshampa mkapata wa miaka mwili raia huyo wa Uganda, imekuwa katika mazungumzo ya kumsajili Kessy licha ya kuwa Mtibwa imekuwa ikiweka ngumu, kuna uwezekano wa kukubali kutokana na mchezaji mwenyewe kuonyesha nia ya kukubali dili.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, alifunguka kuwa mazungumzo yanaendelea vizuri na kama kila kitu kitaenda vizuri, kuna uwezekano wa usajili huo kukamilika ndani ya siku chache zijazo.

“Tupo katika mazungumzo ya mwisho na mchezaji wa Mtibwa, Kessy ambapo wakati wowote kuanzia sasa tutamalizana naye kwa kuingia mkataba mara baada ya kufikia makubaliano na uongozi wake,” alisema Hans Poppe.

Mkurugenzi wa Mtibwa Sugar, Jamal Bayser, alisema ni kweli mazungumzo yanaendelea.

“Tumezungumza na Simba, lakini bado hatujakubaliana, nia yetu haikuwa kumuuza mchezaji yeyote kwa sasa lakini inavyoonekana hata yeye mwenyewe (Kessy), ameonyesha nia ya kutaka kwenda Simba, hivyo tutakujulisha nini kinachoendelea,” alisema kiongozi huyo.

Wakati huohuo, mchakato wa Simba kumuwania beki mwingine wa timu hiyo, Salim Mbonde, umeendelea lakini dalili zinaonyesha kuwa Mtibwa imegoma katakata kumuuza mchezaji huyo.


Taarifa kutoka Mtibwa zinaeleza kuwa klabu hiyo inahofia kuuza wachezaji wake muhimu kwa kuwa ligi bado inaendelea, hivyo suala la kumuuza mchezaji huyo kwa sasa wamelifuta rasmi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic