December 5, 2014


Uongozi wa Simba umechukua uamuzi wa kusitisha kumsajili mshambuliaji Danny Mrwanda wa Polisi Morogoro.


Simba imefikia uamuzi huo baada ya kugundua hakusema ukweli kuhusiana na mkataba wake na Polisi Morogoro.

Habari za uhakika zimeeleza, Mrwanda hakuiambia Simba kama mkataba wake unamzuia kusaini hapa nchini lakini unamruhusu kwenda nje ya Tanzania bila ya kipingamizi.

“Polisi Moro walipiga simu Simba kuwauliza malipo yao, hiyo ikawashitua kwa kuwa walikuwa hawajasaini na Mrwanda hakuwaambia kama Polisi wanatakiwa kulipwa,” kilieleza chanzo.

Alipotafutwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, alithibitisha hilo kwa kusema: “Tumemwambia akazungumze na uongozi wa Polisi, wamalizane na kumpa barua ya kumruhusu.

“Ikiwa hivyo tutamsainisha, isipokuwa hivyo, basi tutafanyaje. Maana hakutuambia vizuri mwanzo kuhusu hilo.”



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic