December 5, 2014


Kumekuwa na taarifa zinazotofautiana kuhusiana na kuchelewa kwa mshambuliaji Emmanuel Okwi aliye kwao Uganda, lakini ukweli sasa suala la ndoa, ndilo lililomchelewesha.

Uchunguzi umeonyesha Okwi yuko katika mipango ya kutaka kufunga ndoa.
Lakini ikawa vigumu kupata uhakika kwa kuwa vyanzo vyetu havikuweza kumpata Okwi jijini humo.

Lakini Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, akakata mzizi wa fitina kwa kulitolea ufafanuzi suala hilo.

Hans Poppe amesema Okwi amepewa ruhusa ya kushughulikia masuala yake na hasa hilo la ndoa.
“Anatarajia kufunga ndoa mwezi huu, nafikiri itakuwa tarehe ishirini, ndiyo maana tumempa ruhusa.

“Ila atarudi kuungana na wenzake kwa ajili ya mechi ya Nani Mtani Jembe dhidi ya Yanga. Baada ya hapo, tutamruhusu tena,” alisema Hans Poppe.

Taarifa za kutoka Kampala zinaeleza, Okwi anamuoa mpenzi wake wa siku nyingi na maandalizi yako katika hatua za mwisho kabisa.

“Kila kitu kiko vizuri, mambo yako katika hatua za mwisho kabisa,” kilieleza chanzo kutoka Kampala.

Tayari Simba imeanza maandalizi kwa ajili ya  Ligi Kuu Bara na Okwi na Joseph Owino ambaye amepata msiba ndiyo walikuwa hawajajiunga na wenzao.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic