December 5, 2014


Kipa wa Azam FC, George Munishi ametua kwenye mazoezi ya Yanga kwa ajili ya kufanya majaribio ya kuichezea timu hiyo inayojiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara na mechi ya Nani Mtani Jembe.


Munishi ni mdogo wake na kipa namba moja wa Yanga, Deogratius Munishi ‘Dida’, tayari amefanya mazoezi kwa siku mbili juzi Jumatano na jana Alhamisi chini ya kocha wa makipa, Juma Pondamali.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani ya benchi la ufundi la timu hiyo, kipa huyo anaangaliwa uwezo wake ndani ya uwanja na kama akiwashawishi viongozi basi watamsajili, ikiwa ni siku chache tangu kuwepo na taarifa kuwa klabu hiyo inaweza kutoendelea kuwa na kipa Juma Kaseja ambaye haonekani mazoezini.

“Benchi la ufundi limetoa nafasi kwa makipa kwa ajili ya kuwasajili katika dirisha dogo na yule atakayeushawishi uongozi atapewa mkataba wa kuichezea Yanga.

“Tayari kipa George ambaye ni mdogo wake Dida, ametua kwenye mazoezi ya Yanga kwa siku mbili mfululizo kwa ajili ya kufanyiwa majaribio,” kilisema chanzo hicho.

Alipoulizwa Dida kuhusiana na hilo, alisema: “Ni kweli kabisa mdogo wangu George ameanza mazoezi na Yanga na tayari amefanya kwa siku mbili, kabla ya kufanya majaribio Yanga alikuwa akiichezea Azam FC ya U14.

“Ana umri wa miaka 16, anasoma Shule ya Sekondari ya Chamazi, aliondoka Azam FC baada ya kubanwa na masomo yake,” alisema Dida.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic