January 26, 2015


Kitendo cha beki wa Ruvu Shooting, George Michael kumpiga kabala ya koo mshambuliaji wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe hivi karibuni wakati timu hizo zilipokutana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, kimeendelea kuwa gumzo na sasa kimevuka mipaka ya Tanzania.


Nchini Burundi anakotokea Tambwe, jambo hilo limekuwa gumzo kubwa lakini pia baadhi ya wachezaji wanaocheza ligi kuu ya nchi hiyo, wamekuwa wakitumiana kwa njia ya mtandao picha ambazo zilipigwa na gazeti hili zikimwonyesha Tambwe akipigwa kabali na Michael.

Mchezaji wa zamani wa Inter Stars ya Burundi, Ndayishimiye Duni, alisema kuwa kitendo hicho kiliwashangaza watu wengi nchini humo, hususan wachezaji.

Alisema kila mtu anaona kuwa, Tambwe hakutendewa haki na beki huyo kwa kumpiga kabala, jambo ambalo ni kinyume na taratibu za soka, hivyo wanalitaka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kumchukulia hatua.

“Lakini pia maneno ambayo alikuwa akitukanwa na beki huyo, kwa kumuita mkimbizi pia siyo mazuri, yanalichafua soka la Tanzania na kuonekana halina Fair Play.

“Hata hivyo wachezaji wengi nchini hapa wamewasiliana na Tambwe na kumpatia pole kutokana na tukio hilo baada ya kuona picha ambazo tulizipata kutoka katika mtandao wa Gazeti la Championi (Global Publishers),” alisema Duni.


Alipoulizwa Tambwe juu ha suala hilo, alisema: “Ni kweli kabisa wachezaji wengi kutoka Burundi wamekuwa wakinipigia simu na kunipatia pole kutokana na jambo hilo.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic