Benchi limetajwa ndiyo
chanzo cha beki wa kati wa Simba Mganda, Joseph Owino kuchukua maamuzi ya
kurudi kwao na kuiacha timu hiyo inayoendelea na michuano ya Kombe la
Mapinduzi.
Beki huyo, hivi karibuni
alirejea nyumbani kwao Uganda mara baada ya kumalizika mechi ya Ligi Kuu Bara
dhidi ya Kagera Sugar iliyomalizika kwa Simba kufungwa bao 1-0 huku Owino
akianzia benchi.
Wakati hali hiyo
ikiendelea, zipo tetesi kuwa beki huyo aliyebakisha miezi sita kwenye mkataba
wake, amepangwa kuondolewa kwenye usajili wa msimu ujao wa ligi kuu ili nafasi
yake ichukuliwe na Mkenya, Paul Kiongera ambaye anaendelea na matibabu.
Kwa mujibu wa chanzo cha
habari kutoka kwa rafiki wa karibu wa beki huyo, Owino hana matatizo yoyote ya
kifamilia yaliyomsababishia arejee kwao zaidi kukerwa na kitendo cha yeye
kuwekwa benchi.
Chanzo hicho kilisema, beki
huyo alianza kushtukia kwenye mechi ya Nani Mtani Jembe dhidi ya Yanga
iliyochezwa Uwanja wa Taifa na mechi kumalizika kwa Simba kushinda mabao 2-0
ambayo alianzia benchi lakini baadaye akaingia.
“Ugumu wa namba kwa Owino ulianza baada ya timu hiyo
kumsajili Musheed (Juko) katika usajili wa dirisha dogo kwa ajili ya
kukiboresha kikosi hicho.
“Wakati anasajiliwa beki
huyo, Owino alijua kwamba yeye watacheza pamoja, lakini baadaye mambo
yakabadilika na nafasi yake kupangwa Isihaka (Hassani).
“Kwa mujibu wa Owino, yeye
alikuwa ameshtukia kuwepo na mipango kutoka kwa mmoja wa viongozi wa juu wa
timu hiyo ambaye yeye hamtaki Owino, hivyo akaona ni vyema aondoke zake ili
awapishe mabeki hao waendelee kuichezea Simba,”kilisema chanzo hicho.
Alipoulizwa Katibu Mkuu wa
timu hiyo, Stephene Ally kuhusiana na beki huyo alisema kuwa: Owino aliomba
ruhusu baada ya kumalizika mechi dhidi ya Kagera.”








0 COMMENTS:
Post a Comment