January 7, 2015

HENRY (KULIA) WAKATI AKIWA SIMBA
Kiungo mkongwe wa Mtibwa, Henry Joseph amefunguka kuwa hata yeye amekuwa haelewi kwanini Simba ilimuacha.

Henry ametua Mtibwa katika usajili wa dirisha dogo msimu huu huku akiwa mwiba kwa Simba baada ya kuifunga katika mchezo wa awali wa Kombe la Mapinduzi linaloendelea huko Zanzibar katika ushindi ambao timu yake ya Mtibwa ilipata wa bao 1-0.

Henry alisema kuwa anashukuru amekuwa katika kiwango kikubwa kwa sasa na amekuwa msaada kwa timu yake ya Mtibwa lakini anashindwa kuelewa Simba ilifikiria nini wakati ule mpaka ikafikiria kumuacha wakati bado msaada wake ulikuwa ukihitajika.


“Nashukuru nimeendelea kudumu kwenye kiwango changu muda wote, nafikiri ni kujitambua tu ndiyo kimesaidia ila huwa nashangaa sijui kwanini Simba iliamua kuniacha wakati ule, sijajua walikuwa wanafikiria nini, ila hayo yamepita kwa sasa ninaangalia jinsi ya kuisaidia timu yangu mpya,” alisema Henry kiungo wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic