January 13, 2015


Kocha wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amekumbana na balaa mjini Musoma.


Julio amepigwa jiwe na kujeruhiwa wakati timu yake ya Mwadui FC ikicheza mechi ya Ligi Daraja la Kwanza dhidi ya Polisi Mara.

Mechi hiyo ilichezwa wikiendi mjini Musoma na kumalizika kwa sare ya mabao 2-2.

Hali hiyo ilisababisha mashabiki wa Polisi kuanza kuwashambulia Julio na wachezaji wake ambao baadhi walijerudiwa.

“Kweli nimepigwa jiwe la mgongoni na sasa siko vizuri. Nimeshindwa hata kwenda mazoezini.


“Hakika hawakututendea haki na askari polisi hawakuwa na msaada,” alisema Julio.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic