January 25, 2015


Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic amekubali kuwa kikosi cha Azam FC ni kati ya vilivyo bora nchini katika soka.


Lakini akahoji, nani ambaye anasema Simba ina kikosi dhaifu na haiwezi kuifunga Azam leo?

Simba na Azam FC zinakutana leo katika mechi ya “big match” za Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Kocha huyo raia wa Serbia amesema, kikosi chake kina uwezo mkubwa wa kupambana.

“Tunataka kupambana na kushinda, tunataka pointi tatu kwa ajili ya kujiweka vizuri kwenye msimamo.


“Lakini vizuri tushinde ili kuondoa hizo hisia kikosi chetu ni dhaifu, njoo uone tunacheza,” alisema

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic