January 23, 2015


Baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutangaza kumfungia mshambuliaji wa Stand United, Haruna Chanongo kucheza mechi tatu na kutakiwa kulipa faini ya shilingi 500,000 kwa madai ya kumpiga teke mwamuzi katika mchezo dhidi ya Polisi Moro, uongozi wa Stand umekata rufaa kupinga.


Mkurugenzi wa Benchi la Ufundi la Stand, Muhibu Kanu amesema wamesikitishwa na maamuzi hayo, ndiyo maana wameamua kukata rufaa kwa kuwa Chanongo hakumpiga mwamuzi huyo teke.

Alisema wameshatuma video ya mchezo huo na barua kwenda kwa kamati ya nidhamu ya TFF ili kupitia video kwa umakini.

“Chanongo ni mchezaji mzoefu, hawezi kufanya kitu kama hicho, tunaamini haki itatendeka,” alisema.


Hata hivyo, marudio ya picha za runinga katika mechi hiyo hayakuonyesha kama Chanongo alimpiga teke mwamuzi huyo.

Hivyo TFF inaweza kuwa na deni la kuthihirisha hilo kama kweli lilitokea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic