January 23, 2015



Saa zaidi ya 24 baada ya Yanga kutishia kugomea kuingiza timu uwanjani, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema endapo klabu hiyo itathubutu kufanya hivyo, basi itakutana na rungu la sheria kali za Ligi Kuu Bara.


Yanga ilitoa tamko hilo, ikishinikisha TFF iwachukulie hatua kali waamuzi wa mchezo wao dhidi ya Ruvu Shooting, wachezaji wa Ruvu waliomchezea ‘kibabe’ straika wao, Amissi Tambwe.
 
Selestine Mwesigwa ambaye ni Katibu wa TFF, ameliambia gazeti hili kuwa, wao wanasubiri taarifa ya maandishi na hawawezi kufanya kazi kwa shinikizo.

“Kuhusu suala la kugoma, nafikiri Yanga wanaelewa kila kitu kuhusu sheria, kanuni na taratibu za ligi, kama kuna malalamiko, wao wanajua waende wapi.

“Kuhusu kutoa maamuzi ya mchezo wa Yanga na Ruvu, hatuwezi kuzungumza lolote kwa kuwa hatujapata ripoti husika ya mchezo.

“Kuhusu ripoti ya kamishaa kuwekwa wazi hilo halitawezekana kwa kuwa hiyo siyo taratibu, kama hii ikiwekwa wazi ina maana basi kila ripoti itabidi iwekwe wazi,” alisema Mwesigwa.


Tambwe alikutana na shuruba hiyo katika mechi ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa Jumamosi iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa ambapo alikuwa na wakati mgumu katika kumpita beki wa Ruvu, George Michael.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic