January 7, 2015


Mshambuliaji wa Simba Dan Serrunkuma amegeukwa na mashabiki wa timu hiyo baada ya kupokelea kama mfalme kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi.


Sserunkuma alisajili na Simba akitokea Gor Mahia ya Kenya baada ya kuibuka mfungajili bora wa Ligi Kuu ya nchi hiyo, lakini ameshindwa kuendeleza cheche zake kwa Wekundu hao wa Msimbazi.

Juzi Jumapili mchezaji huyo alionja joto ya jiwe baada ya kuzomewa na mashabiki kutokana na kuonyesha kiwango kibovu kwenye mchezo dhidi ya JKU ya visiwani hapa ambao Simba walipata ushindi wa bao 1-0.

Hata hivyo kitendo hicho kuzomewa mchezaji huyo kilimsikitisha mchezaji huyo ambaye alisema kwamba:

 “Ila soka ndiyo hivyo lilivyo lakini naomba niwaambie mashabiki wa Simba kuwa wawe na subira mambo yatakuwa vizuri tu japokuwa kwa sasa sijisikii vizuri,” alisema Sserumkuma.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic