February 9, 2015

Watu 22 wamepoteza maisha katika vurugu za uwanjani nchini Misri na Shirikisho la Soka la Misri limetangaza kuisimamisha ligi kuu nchini humo kwa muda usiojulikana.

Watu hao wamepoteza maisha baada ya kutokea vurugu kati ya polisi wa Misri dhidi ya mashabiki wa zamalek.

Msemaji wa Wizara ya Afya ya Misri, Hossam Abdel Ghafar, ametangaza watu watano wameuwawa katika vurugu hizo zilizohusisha mechi kati ya Zamalek dhidi ya ENPPI.

Ghafar amesema pamoja na watu hao watatu kuuwawa, wengine 34 wamejeruhiwa na wako hospitali wanakopata matibabu.

Lakini taarifa za vyombo vya habari zinaeleza, watu 22 wamepoteza maisha katika tukio hilo.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic