February 7, 2015


Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva na beki wa pembeni wa Mtibwa Sugar, David Luhende, kila mmoja kwa muda wake ametoa vitisho vya kuhakikisha anamzimisha mwenzake katika mechi baina ya timu hizo kwenye Ligi Kuu Bara, kesho Jumapili.


Yanga inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mtibwa kwenye Uwanja wa Taifa, ambapo Msuva ndiye amekuwa staa wa Yanga katika siku za hivi karibuni huku Luhende ndiye beki wa Mtibwa ambaye anaweza kukutana naye mara kwa mara ikiwa wote watacheza mechi hiyo.

Msuva ameliambia gazeti hili kuwa, yupo fiti kupambana na beki yeyote atakayekutana naye bila kujali ni Luhende au mwingine.

“Nikwambie ukweli tu, mimi nikiamua jambo langu uwanjani, hakuna mchezaji yeyote atakayenizuia, hivyo huyo beki wa Mtibwa atakayepangwa basi anatakiwa ajiandae.

“Kama atapangwa kuanza Luhende, itakuwa vizuri kwangu kwa sababu ninamjua vizuri, nitamtia hasira tu kwa kumpiga chenga za maudhi na kukokota mpira kwa kasi kwa ajili ya kumchosha,” alisema Msuva.

Upande wa Luhende ambaye ni mchezaji wa zamani wa Yanga, alisema: “Mimi hakuna mshambuliaji ninayemhofia, nimejiandaa vizuri na mechi hiyo dhidi ya Yanga, sitaki kuongea sana, tuonane uwanjani.”



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic