February 16, 2015

Kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti sasa atakuwa na amani moyoni kwa kuwa beki wake, Pepe amerejea.


Kwa mujibu wa kitengo cha afya cha Real Madrid, Pepe sasa yuko poa na anaweza kucheza mechi zinazofuata.

Pepe ambaye kuumia kwake kulifanya safu ya ulinzi ya Real Madrid iyumbe kinoma, sasa amerejea.

Amekuwa akiaminika kama kiongozi wa safu ya ulinzi ya Madrid akisaidiana na Sergio Ramos.


Jumatano, Madrid itakuwa na kazi ngumu ya kuivaa Schalke 04 ya Ujerumani na watakuwa na nguvu zaidi kutokana na kurejea kwa beki huyo kisiki.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic