Kocha
wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ametua katika kikosi cha Coastal
Union na kuanza kazi.
Julio
anatua Coastal kama sehemu ya ‘urafiki’ wake na klabu hiyo ili kusaidia
kuboresha benchi la ufundi.
Tayari
Coastal Union iko chini ya Kocha Mkenya, James Nandwa lakini mwendo wake
umeonekana kutowaridhisha Wanatanga.
Julio
alitua kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga na kuzungumza na wachezaji.
Kabla
ya hapo alifanya mazungumzo na viongozi wa Coastal Union.
0 COMMENTS:
Post a Comment