Rais
wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amepeleka salamu za rambirambi kwa
familia ya Mohamed Nyama, kufuatia kifo cha mwamuzi mstaafu Mohamed Nyama ambaye
pia aliwahi kuwa mjumbe wa kamati ya waamuzi ya TFF kilichotokea jana
kwao Nachingwea- Lindi.
Marehemu Nyama wakati wa uhai wake alikuwa mwamuzi wa daraja la kwanza ambaye
pia alitambuliwa na FIFA, Nyama anatarajiwa kuzikwa leo jioni kwao Nachingwea
mkoani Lindi na TFF
itawakilishwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Athumani
Kambi.
Katika
salam zake kwa familia ya Nyama, kwa niaba ya TFF, familia ya mpira wa miguu na
watanzania Rais Malinzi amewapa pole wapenzi wa mpira wa miguu nchini
katika kipindi hiki kigumu cha maombelezo.
0 COMMENTS:
Post a Comment