March 30, 2015


Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Mbrazili, Andrey Coutinho, ambaye hajaonekana uwanjani kwa muda mrefu, leo Jumatatu anatarajiwa kuanza mazoezi mepesi kutokana na hali yake kuendelea kuimarika.


Coutinho amekaa nje ya uwanja kwa wiki tano akiuguza goti. Aliumia katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mbeya City Februari 24, mwaka huu ambapo Yanga ilishinda 3-1.

Coutinho amesema kuwa anamshukuru Mungu kwani hali yake inaendelea vizuri.

“Ninamshukuru Mungu kwani hali yangu inaendelea vizuri na inaleta matumaini, hivyo kesho Jumatatu ninaanza mazoezi mepesi kutokana na ripoti ya daktari wangu,” alisema.


Alipomtafutwa daktari wa Yanga, Juma Sufiani, ili kuhakikisha taarifa hizo alisema: “Ni kweli Coutinho anaendelea vizuri ambapo kesho (leo) nimemruhusu aanze mazoezi mepesi ili kuimarisha zaidi viungo vyake.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic