March 30, 2015

TENGA
Rais wa TFF, Jamal Malinzi amesema Tanzania itampigia kura ya ushindi Rais Sepp Blatter wa Fifa.


Lakini Rais wa Cecafa, Leodeger Tenga naye ameungana na Malinzi na kuamini huo ni msimamo sahihi.
 
MALINZI
Kwa maneno hayo, maana yake Tanzania tayari imeweka wazi kuhusiana na msimamo wake wa kutompigia kura Luis Figo ambaye ametangaza kupambana na Blatter.

Figo raia wa Ureno aliyeng’ara katika soka akiwa na timu za Barcelo, Real Madrid na Inter Milan, hatapata kura ya Tanzania.

Lakini kwa maneno ya Tenga, inaonekana atakuwa na kazi ya kupata kura upande wa bara la Afrika.

Malinzi na Tenga wamesema Blatter amekuwa na msaada mkubwa kwa Afrika kuhakikisha wanatimiza ndoto zao kwa maendeleo ya soka.


Hata hivyo hakuweka wazi nini hasa ambacho amekuwa akijitolea kuisaidia Tanzania au Afrika!

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic