Mwamuzi
wa kimataifa wa Tanzania mwenye beji ya Fifa, Israel Mjuni Nkongo amechaguliwa
kuchezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya wenyeji Zesco FC ya
Zambia dhidi ya AS Kaloum ya Guinea.
Katika
mchezo huo wa kwanza wa mzunguko wa pili, Nkongo atasaidiwa na washika
kibendera John Kanyenye na Josephat Bulali na mwamuzi wa akiba Waziri Sheha
wote kutoka Tanzania, huku Kamisaa wa mchezo akiwa Mayixole Elvin Shishana
kutoka nchini Afrika Kusini
Mchezo
huo unatarajiwa kufanyika kati ya tarehe 13,14,15 Machi mwaka huu nchini Zambia
0 COMMENTS:
Post a Comment