March 2, 2015


Baada ya juzi Jumamosi Simba kulala na furaha kutokana na kuipa kichapo cha mabao 5-0 timu ya Prisons ya Mbeya, jana haikutaka kulaza damu, badala yake ikasafiri kuelekea Zanzibar kuweka kambi kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao dhidi ya Yanga.




Simba inatarajia kuwavaa mahasimu wao hao wakubwa katika Ligi Kuu Bara Jumapili ijayo, Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Imekuwa ni kawaida kwa timu hiyo kwenda kuweka kambi visiwani Zanzibar kila inapokuwa na michezo migumu ya ligi mbele yake, hasa dhidi ya Yanga. Taarifa zinasema timu hiyo itarejea Jumamosi, tayari kwa mchezo huo.

Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola, alisema timu hiyo imeondoka jana majira ya saa sita mchana lakini yeye na Kocha Mkuu, Mserbia, Goran Kopunovic wanatarajia kuondoka leo kujiunga na timu hiyo kutokana na sababu mbalimbali.

“Timu inaondoka leo (jana) na itarejea Jumamosi ila bado hatujajua kuhusu mechi za kirafiki, lakini kuhusu mimi na kocha Kopunovic, tutaondoka kesho (leo) kwa kuwa kule mazoezi rasmi yataanza kesho hiyohiyo, ilibidi tuondoke wote kwa pamoja kesho (leo) lakini ikaangaliwa na uzito wa mechi yenyewe, tukaona bora timu iwahi kwanza,” alisema Matola.
Katika mchezo wa awali wa ligi, timu hizo zilitoka suluhu lakini baadaye Simba ilishinda 2-0 kwenye mchezo wa kirafiki wa Nani Mtani Jembe 2.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic