March 2, 2015





 Donald Ngoma wa FC Platinum (kushoto) akiwa katika harakati zake uwanjani.

Na Louis Ngwako, Gaborone

Watanzania wanaoishi mjini hapa, wametoa tahadhari kubwa kwa kikosi cha Yanga kabla ya kuivaa FC Platinum ya Zimbabwe.

Mashabiki hao wamemtaka Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm kuwa makini na mshambuliaji Donald Ngoma wa FC Platinum.

NGOMA (KUSHOTO) AKIPAMBANA UWANJANI...
FC Platinum itakutana na Yanga Machi 14, mwaka huu katika mechi inayofuata ya Kombe la Shirikisho baada ya kuing’oa Sofapaka ya Kenya kwa kuifunga nyumbani na ugenini.

Wakizungumza jijini hapa, wameliambia Championi Jumatatu kuwa Ngoma amekuwa hatari sana kila anapokutana na timu za Botswana.

“Tumeona akicheza na timu za Botswana, jamaa ni hatari, anavaa jezi namba kumi na moja. Ana kasi, anapiga mashuti sana.

“Hata mechi mbili dhidi ya Sofapaka ya Kenya, zote amefunga. Lazima wamchunge, pia ni mjanja sana hata kama yuko katikati ya mabeki wa timu pinzani,” alisema Mtanzania aliyejitambulisha kwa jina moja la Humphrey huku akiungwa mkono na wenzake.

Ngoma amekuwa tegemeo katika safu ya ushambuliaji ya FC Platinum inayoonyesha kupania kusonga mbele zaidi. Platinum iliifunga Sofapaka kwa mabao 2-1 katika kila mechi na kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-2.

Yanga ndiyo timu pekee ya Tanzania iliyofanikiwa kusonga mbele katika michuano ya kimataifa, baada ya kufanikiwa BDF ya Botswana kwa jumla ya mabao 3-2.

Mabao mawili ya straika Amissi Tambwe yaliibeba Yanga katika ushindi wa 2-0 Dar es Salaam, wakati bao moja la Mrisho Ngassa kwenye kipigo cha juzi cha 2-1, ndilo lililosaidia kuivusha timu hiyo katika hatua ya kwanza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic