April 10, 2015

Wakati bondia wa ngumi za kulipwa Mtanzania, Mohammed Matumla akishindwa kupata majibu ya kama atakwenda kuzichapa nchini Marekani au la, taarifa rasmi zinaonyesha nafasi hiyo amepewa bondia kutoka Morocco, Said El Harrack.


Licha ya ushindi dhidi ya Mchina, Wang Xin Hua, lakini promota aliyesimamia pambano la Matumla na Mchina, Jay Msangi, amesema safari ya Matumla imeshindikana kwa kuwa ameshindwa kufikia vigezo vilivyowekwa na waandaji wa pambano la Manny Pacquiao dhidi ya Floyd Mayweather.

“Suala la Matumla kwenda Marekani ilikuwa ni moja ya ahadi zetu iwapo atashinda na tulituma mkanda wa video kwa meneja wa Pacquiao ambaye ndiye ameupeleka kwa waandaaji ambao wao wanaamini kwamba Matumla hawezi kupigana siku hiyo kwa kuwa hakufikia vigezo wanavyotaka wao.

“Sababu kubwa waliyoitoa wao ni kwamba Matumla alishindwa katika mapambano yake mawili ya nyuma, pia katika pambano dhidi ya Mchina alicheza faulo nyingi, sasa wao wameona ni vema nafasi hiyo apewe huyo Mmorocco kwa sababu ameweza kukidhi vigezo,” alisema Jay Msangi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic