April 12, 2015


Unaweza kuona kama maajabu, Kamati ya Rufaa ya TFF imekutana leo kukaa kusikiliza rufaa ya Dk Damas Ndumbaro, bila ya kumtaarifu.


Taarifa za uhakika zimeeleza kamati hiyo imekaa leo jijini Dar es Salaam kusikiliza rufaa ya Dk Ndumbaro kupingwa kufungiwa kujihusisha na masuala ya soka kwa miaka mitano.

“Kweli tuko, tumekaa kwenye kamati na ukweli nikieleza Dk Ndumaro hajaitwa na hajui lolote,” kilieleza chanzo kutoka ndani ya kamati hiyo.

“Unajua kinachoonekana kama TFF hawakutaka kamati  ikae, huenda kuna shinikizo ili kutenda haki. Hivyo umefanyika ujanja Dk Ndumbaro asiitwe.

“Hiki ni moja ya mambo ya ajabu kutokea katika soka, nilipofika hapa na kugundua Dk Ndumbaro hajaitwa kwa kweli imenisikitisha sana.”

SALEHJEMBE ilimtafuta Dk Ndumbaro ambaye alisema amepata taarifa hizo kupitia kwa rafiki yake.

“Kwa kweli mimi bado naona haya ni maajabu katika soka. Nashangazwa sana na kinachoendelea kutokea, nimepewa taarifa na mtu, aliniuliza jana, nikamuambia hawawezi kukaa bila ya kujipa taarifa.

“Mimi ndiyo mlalamikaji, watakaaje bila ya kuniambia, si lahisi. Leo mtu kaniambia ndiyo kwenye kikao wanasikiliza rufaa yangu, hii ni ajabu kabisa.

“Kutoka ofisini kwangu na ofisini kwa katibu wa TFF ni mwendo wa dakika tano. Lakini sijapewa taarifa kuwa na kikao cha rufaa yangu.

“Sitaki kusema maneno mengi sana, lakini kupitia hili wadau wa soka wataona namna kulivyo na mambo ya kushangaza ambayo hayapaswi kuvumiliwa.


“Sina hofu, naendelea kusubiri kwa kuwa sijui mfumo uliotumika,” alisema Ndumbaro ambaye ni daktari wa sheria.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic