April 24, 2015

Beki wa Simba, Abdi Banda anashikiliwa na Jeshi la Polisi Tanzania kwa tuhuma za kushiriki upotevu wa gari lililoibiwa.


Habari za uhakika zilizoifikia SALEHJEMBE zimeeleza kuwa Banda anashikiliwa pamoja na mdogo wake kwa tuhuma za wizi wa gari linalomilikiwa na mwanamke mmoja aliyeelezwa kuwa ni mpenziwe.

Ingawa viongozi wa Simba wamekuwa wagumu kupatikana na kuzungumzia suala hilo, lakini SALEHJEMBE imethibitisha Banda ameshikiliwa kituoni hapo tokea jana usiku.

Mmoja wa askari wa kituo cha Magomeni amethibitishwa kushikiliwa kwa beki huyo mwenye uwezo wa kucheza kama kiungo na uchunguzi unaendelea.

“Kweli yuko kituoni anashikiliwa, anashikiliwa yeye na mdogo wake kuhusiana na kuibiwa kwa gari la dada mmoja anayeelezwa ni mpenzi wa mchezaji huyo,” alisema.

Taarifa zinaeleza Banda amekuwa akilianzima gari hilo na kulitumia kila mara.

“Kweli amekuwa akilitumia gari hilo lakini yeye hajui kuendesha. Mdogo wake amekuwa akiendesha gari hilo na kuna mkanganyiko wa taarifa.

“Inaelezwa wakati linapotea yeye alikuwa jijini Mbeya Simba ilipokwenda kuivaa Mbeya City. Lakini mmiliki wa gari anasisitiza Banda ndiye alilianzima kupitia mdogo wake. Hivyo tumewaachia polisi wafanye kazi yao,” alieleza ndugu wa Banda.

Viongozi wa Simba walikuwa hawapokei simu zao lakini ilielezwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Stephen Ally alikuwa katika kituo hicho cha Magomeni akilishughulikia suala hilo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic