April 7, 2015



Makamu wa Rais wa klabu hiyo, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ alijikuta akilazimika kufanya kazi ya ziada kusaidia kumbembeleza kiungo Jonas Mkude katika msiba wa baba yake mzazi.


Mkude alikuwa ni mtu mwenye uchungu, alishindwa kujizuia na kulia kwa nguvu hali iliyomfanya Kaburu amsogelee na kuanza kuzungumza naye akimshawishi kuwa mvumilivu.

Hata hivyo, Mkude alishindwa kujizuia na kuzidi kulia akionyesha kuhuzunisha watu wengi pale msibani.

Kuona hivyo, Kaburu alichukua uamuzi wa kumkumbatia na kumueleza maneno kadhaa ambayo angalau yalionyesha kumtuliza.

Baba yake alifariki juzi na kumlazimisha Mkude kuondoka kambini Simba mjini Shinyanga kurejea jijini Dar.


Maziko yamefanyika katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic