April 7, 2015

 Baba wa kiungo wa Simba, Jonas Mkude amezikwa leo katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Gerrard Mkude amezikwa leo kwa ushirikiano mkubwa wa ndugu, jamaa na marafiki waliojitokeza leo.
 
ABDI BANDA (WA PILI KUSHOTO) AKIWA KATI YA WAOMBOLEZAJI.

Msiba huo ulikuwa Kinondoni Studio nyumbani kwa marehemu ambapo ibada ilifanyika kabla ya kwenda makaburini.
Uongozi wa Simba uliwakilishwa na Makamu wa Rais wa klabu hiyo, Geofrey Nyange ‘Kaburu huku upande wa wachezaji wakiwakilishwa na Abdi Banda na kwa makocha alikuwepo Kocha Msaidizi, Selemani Matola.

Mashabiki kadhaa, majirani na marafiki wa familia ya Mkude walijitokeza kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic