April 7, 2015

GARCIA AKIFANYIWA MAHOJIANO NA WAANDISHI JIJINI DAR ES SALAAM, LEO.
Mshambuliaji hatari wa zamani wa Barcelona na Liverpool, Luis Garcia amesema wanataka ushindi katika mechi dhidi ya nyota wa Tanzania kwenye Uwanja wa Taifa, Jumamosi.

AKIZUNGUMZA NA 'BONGE' SALEH ALLY...
Garcia amesema kikosi cha wakongwe wa Barcelona kina wachezaji wengi bora ingawa wanajua utakuwa mchezo mgumu.

Akizungumza na SALEHJEMBE jijini Dar es Salaam, Garcia amesema yeye na baadhi ya wachezaji wameishawasili jijini Dar.

“Tutakuwa hapa Tanzania tukisubiri mchezo huo, tumeambiwa kwamba kikosi cha Watanzania ni kizuri.
“Hivyo tumeijiandaa na tunajua haitakuwa kazi lahisi lakini tunachotaka ni ushindi,” alisema.

Garcia aliwahi kuichezea Barcelona katika kikosi kimoja na Ronaldinho.


Wachezaji wengine watakaokuwa katika kikosi kitakachocheza Jumamosi ni pamoja na Mandieta, Patrick Kluivert, Deco na wengine ambao imeelezwa watatajwa baadaye.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic