April 8, 2015

AMRI SAID
Baada ya Polisi Morogoro kukubali kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa maafande wenzao wa Mgambo JKT, kocha wa timu hiyo, Amri Said ‘Jaap Stam’, amewatupia lawama mabeki wake kwa kusema kuwa ndiyo waliosababisha kichapo hicho.


Mgambo wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani, Mkwakwani, waliweza kuishushia Polisi Moro kipigo hicho, kwa mabao ya Full Maganga, Salum Gilla na Malimi Busungu aliyepiga mawili.
 
POLISI MOROStam amesema kipigo hicho ni kutokana na uzembe mkubwa uliofanywa na mabeki wake.


 “Timu ilicheza vizuri ila mabeki ndiyo walichangia kwa asilimia kubwa tupoteze mchezo huu, wamefanya makosa mengi ya kizembe ambayo wapinzani wetu wameyatumia kutufunga, kama wangekuwa makini tusingepoteza mchezo huu,” alisema Amri Said, mchezaji wa zamani wa Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic