April 8, 2015


Kocha Mkuu wa Yanga, Mdachi, Hans van Der Pluijm, amefunguka na kuelezea sababu ambazo zitamfanya kuwamaliza mapema Waarabu wa Tunisia, Etoile du Sahel, katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.


Yanga ni kama imetupwa kwenye kundi la siafu kwa kukutanishwa na mabingwa hao wa zamani wa Kombe la Shirikisho katika raundi wa pili, ambapo mshindi ataingia hatua ya makundi.

Pluijm amesema anajua ‘nature’ ya soka la timu kutoka Tunisia kuwa zinacheza soka la akili, nidhamu, kiufundi zaidi na kubwa kuliko ni soka la kukaba kila idara.
Katika hilo, Pluijm alisisitiza kuwa wanatakiwa kutumia zaidi faida ya nyumbani kujiwekea akiba ya mabao, vinginevyo wanaweza kujikuta pabaya.

“Kikubwa tunahitaji kuwa makini, kucheza kitimu zaidi, tukipata mabao yetu ni lazima safu ya ulinzi iwe makini kwa kujipanga zaidi, maana unajua kinachofuata unapokuwa kwenye ardhi yao,” alisema na kuongeza kuwa pia anahitaji kupata CD zao ili kuwajua nje-ndani.


“Moja ya kazi zangu ni kuhakikisha napata data za kutosha kuhusiana nao ili tujipange zaidi, nadhani itasaidia kwa kiasi kikubwa, ingawa tunahitaji maandalizi ya kutosha kama kila kitu tutakifanya kwa umakini, hakika tutawatupa nje.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic