April 8, 2015


Kikosi cha Yanga kitakachoivaa Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, leo kitamkosa kiungo wake mwenye kasi, Mrisho Ngassa, ambaye anasumbuliwa na nyama za paja.


Ngassa alikuwa miongoni mwa nyota waliokosa mazoezi ya jana asubuhi kwenye Uwanja wa Karume, Dar wakijiandaa na mchezo dhidi ya Coastal Union.

Wengine ambao walifika mazoezini lakini hawakujumuika katika mazoezi ya jumla ni Said Juma Makapu na Danny Mrwanda ambaye alikuwa anasumbuliwa na tumbo.

Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm, amesema kuwa Ngassa hataweza kucheza leo.


“Ngassa atapumzika, anasumbuliwa na nyama za paja, hivyo nimemwambia apumzike. Kama ameshindwa kufanya mazoezi na wenzake, maana yake hawezi kucheza mchezo wa kesho  (leo) dhidi ya Coastal Union,” alisema Pluijm.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic