April 11, 2015

 
PATRICK KLUIVERT AKIDHIBITI MPIRA MBELE YA KIPA JUMA KASEJA..
Kikosi cha wakongwe wa Barcelona kimeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya nyota wakongwe wa Tanzania katika mechi ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.


Mshambuliaji Patrick Kluivert ndiye alikuwa shujaa baada ya kufunga mkwaju wa penalti wa bao la pili.

Kluivert alifunga mkwaju huo na kumuacha kipa Juma Kaseja akianguka kushoto kwake na mpira ukiingia kulia.
 
KLUIVERT AKIDHIBITI MPIRA MBELE YA NICO NYAGAWA, HARUNA MOSHI 'BOBAN' NA JOHN MWASASU.
Barcelona walikuwa wa kwanza kufunga bao kupitia kwa Luis Garcia ambaye aliwachambua mabeki wa Tanzania wakongwe na kufunga.

Yusuf Macho ‘Musso’ akafunga baso safi la pili kwa shuti kali katika dakika ya 42. Mabao hayo yalidumu hadi mapumziko.
 
NSAJIGWA AKIMDHIBITI SIMAO SAMBROSA...
Barcelona ndiyo walikosa nafasi nyingi zaidi za kufunga kupitia kwa Garcia na Gaizka Mandieta ambaye alicheza beki wa kulia.



Idadi ya watu uwajani hapo haikuwa kubwa sana na ilielezwa kutokana na tatizo la kutokuwa na matangazo au taarifa ya kutosha kuhusiana na mechi hiyo na wengine walilalama kuhusiana na kiingilio.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic